Sababu kwa nini Barcelona imesajili wakati wamezuiliwa

Watu wengi wanahoji kwa nini Barcelona imesajili na kupata sign ya mchezaji wa zamani wa Sevilla Alex Vidal kwa sasa ni mali ya Barcelona ambae alikuwa moto katika fainali ya europa na kuisadia timu yake hiyo ya zamani kuwa mabingwa kwa msimu wa pili mfululizo na mara baada ya fainali ya mabingwa ulaya kuisha na Barca kuchukua ubingwa kwa ushindi wa goli 3 kwa 1 dhidi ya Juventus Barcelona walifanikiwa kuingia makubaliano na Alex Vidal ambapo jamaa amesaini dili litakalomuweka Camp nou kwa misimu mitano ingawa hatocheza mechi yoyote katika msimu wa kwanza mpaka Barcelona watakapotoka katika kifungo cha kuzuiliwa kusajili lakini mbali na kuzuiliwa kucheza Vidali hatozuiliwa kupokea mshara wake waliokubaliana na Barca na atagonga mpunga wake kama kawa ila hatoweza kucheza mpaka msimu wa pili. Barcelona ilikatazwa kufanya usajili mara baada ya kuvunja sheria ya fifa kusajili wachezaji chini ya umri wamiaka 18 lakin Barcelona hawakuzuiliwa kuingia makubaliano na timu fulani au wachezaji itakaowataka.

Comments

Popular posts from this blog

Bad news for Manchester United Manchester City and Arsenal in UEFA Champions League

State’s financial support to farming reaches 1tri/-